Monday, March 25, 2013

STARS ILIVYOUA WAMOROCCO TAIFA.


 Mshambuliaji wa Timu ya Taifa (Taifa Stars) Thomas Ulimwengu, akichezewa vibaya na beki wa Morocco, wakati wa mchezo wa Kundi C wa Kufuzu kucheza michuano ya Kombe la Dunia 2014 nchini Brazil. Mchezo huo umechezwa leo jioni kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaa, ambapo timu ya Taifa Stars, imeibuka na ushindi wa mabao 3-1 huku bao la kwanza likifungwa na Thomas Ulimwengu katika dakika ya 46, na mabao 2 yakifungwa na Mbwana Samatta katika dakika ya 67 na 80.
 

''Leo Mtanijua tu'', Ni Thomas Ulimwengu akionyesha uwezo mbele ya beki wa Morocco.....
 
 Samatta (kushoto) na Ulimwengu, wakishangilia baada ya kutupia...
 
 Wachezaji wa Stars, wakishangilia bao la pili....
 Sehemu ya mashabiki waliojitokeza kuipa sapoti timu ya Taifa....

No comments:

Post a Comment