Monday, November 24, 2014

AL SHABAB WAKIRI KUTEKA BASI NA KUUA WATU 28 NCHINI KENYA.


Al Shabaab lakiri kutekelza shambulizi nchini kenya
Kundi la Al Shabaab nchini Somali linasema kuwa limefanya mashambulizi ya abiria 28 katika basi moja kazkazini mashariki mwa kenya.
Basi hilo ambalo lilikuwa likiwabeba abiria 60 lilitekwa katika jimbo la mandera lilipokuwa likelekea mjini Nairobi.
Abiria mmoja ambaye alinusurika ameiambia BBC vile raia wasio wa Somali walitengwa na wengine na wale ambao hawakuweza kusoma aya ya Quran walipigwa risasi kwa karibu.
Katika taarifa yake al Shabaab limesema kuwa mashambulizi hayo ni ya kulipiza kisasi mauaji ya waislamu huko Mombasa yaliotekelezwa na vikosi vya usalama vya kenya.
Kenya imekumbwa na misururu ya mashambulizi ya risasi na mabomu yanayodaiwa kutekelezwa na kundi la Alshabaa tangu vikosi vyake viingie nchini Somali.
The bodies of 28 non-Muslims who were executed today by Islamic Shebab lie on the ground in Mandera, before being taken to a nearby hospital
Miili ya watu 28 wasio Waislamu waliotekwa na kikundi cha Shabab ikiwa imelazwa uwanjani mjini Mandera, kabla ya kupelekwa hospitali ya jirani
Among the victims were several children, who were shot in the head at point-blank range alongside the other victims
Miongoni mwa wahanga walikuwa watoto kadhaa ambao walipigwa risasi kichwani

Thursday, November 20, 2014

MKUU MPYA WA MKOA WA DODOMA CHIKU GALAWA AFUNGUA WARSHA YA KUPINGA RUSHWA YA NGONO KATI YA MABOSI NA WATENDAJI WA CHINI.

 Mwenyekiti wa Chama cha Majaji wanawake Tanzania Jaji Engera Kileo
akizungumza katika semina hiyo.
 Wajumbe waliohudhuria warsha ya kutafuta namna ya kukomesha Rushwa ya
ngono maofisini kati ya mabosi watendaji wa chini ikiwemo vyuoni na
mashuleni iliyoandaliwa na chama cha majaji wanawake Tanzania [TAWJA]
iliyofanyika Dodoma
                                      wajumbe wakiwa katika mkutano huo
 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Chiku Galawa akifafanua jambo wakati alipokuwa
akifungua Semina ya siku moja ya kutafuta namna ya kukabiliana na
Rashwa mbalimbali ikiwemo ya Ngono kati ya viongozi na watendaji wa
chini iliyoandaliwa na Chama cha Majaji Wanawake Tanzania [TAWJA].
Mkuu wa Mkoa Chiku Galawa, Mwenyekiti wa Chama cha Majaji wanawake
Tanzania Jaji Engera Kileo na Ofisa Miradi wa UN woman Programe Ofice
Cralissa Berg wakifurahia jambo wakati wa mapumziko mafupi ya semina
ya kutafuta ufumbuzi wa kutokomeza Rushwa ya ngono iliyoandali na
TAWJA.

PICHA NA JOHN BANDA


MMILIKI WA LINAS CLUB BUKOBA AFARIKI AKIFANYA MAPENZI NDANI YA GARI


 Mmiliki wa Club ya Linas ya mjini Bukoba, Leonard Mtensa, akiwa hospitali baada ya kufikishwa hapo akiwa amefariki kwa kile kilichoelezwa na Polisi mkoa kuwa alifariki wakati akiwa katika mahaba na mpenzi wake ndani ya gari.
 Tamko la Polisi mkoa kuhusu kifo hicho.
 Mdada anayedaiwa kuwa mke wa marehemu.
Mke wa marehemu akilia huku akiugusa mwili wa marehemu mumewe wakati ukiwa hospitalini.

Thursday, November 13, 2014

WINDHOEK PARTY NDANI YA NYUMBANI PARK MOROGORO NI BALAAAAAH!


DJ Emmanuel akipagawisha wapenzi wa muziki. 
 Ofisa Mauzo wa Windhoek Kanda ya Kati, Emmanuel Mbaule (kulia), akiwa na mdau wa Windhoek katika club hiyo.
 Warembo hawa nao walikuwepo kupata Windhoek na burudani ya mziki hakika ilikuwa kama usiku wa Windhoek wacha tu wajimwaemwae.
 Hapa wakifurahi baada ya kupata Windhoek 'Chezea Windhoek wewe onja uone' kazi kweli kweli.
Tu tost kidogo jamani tuimarishe afya zetu kwa kunywa 
windhoek. Jamani ni tamu hizo we acha tu.

Monday, November 10, 2014

PICHA MBALIMBALI KATIKA WINDHOEK SUNDAY BONANZA DODOMA ROYAL VILLAGE HOTEL

 wanamuziki wa TNC band wakikonga nyoyo za mashabiki wa windhoek
 wapiga vyombo wa TNC wakicharaza magitaa yao katika windhoek bonanza royal village hotel
 mashabiki mbalimbali waliofurika katika windhoek bonanza royal village hotel dodoma
vimwana wa windhoek wa dodoma wakiwa tayari kwa kutoa huduma

Friday, November 7, 2014

KAMPUNI YA BIA YA MABIBO KUPITIA BIA ZAKE ZA WINDHOEK LAGER NA WINDHOEK DRAUGHT YAJITOSA KUINUA UCHUMI WA MKOA KAGERA

 Mshauri wa Kimataifa wa Kujitegemea, Fr.James Rugemalira akizungumza na wadau mbalimbali wa mjini Bukoba wakati wa Promosheni ya bia za Windhoek Lager na Windhoek Draught katika sherehe za kuadhimisha miaka 20 tangu kuanzishwa kwa Kampuni hiyo zilizofanyika Hoteli ya New Coffee Tree Inn mjini Bukoba leo usiku. (Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com simu namba 0712-727062)
 Fr.James Rugemalira (katikati), akisisitiza jambo
 kwenye promosheni hiyo. Kutoka kushoto ni Mganga
 Mkuu wa Halmsahauri ya Wilaya ya Bukoba, Hamza
 Mugura, Mkurugenzi wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya
 inayofanya shughuli zake mjini Bukoba ya KADETFU,
Yusto Muchuruza, Mshauri wa Fr.James, Enic Kashasha
 na Andrew Kailembo.
 Wadau wakiwa kwenye promosheni hiyo.
 Mrembo huyu mnywaji wa Windhoek naye
 alikuwepo kwenye promosheni hiyo.
Mshereheshaji wa Promosheni hiyo, Andrew Kagya,
 akiwajibika.

 Meneja Mauzo wa Kanda ya Ziwa, Godfrey Mwangungulu, akielezea ubora wa Bia za Windhoek.
Mdau wa Windhoek akifuatilia matukio yote kwa karibu.
 Hakika imependeza.

Fr.James Rugemalira (katikati), akiwa meza kuu na viongozi mbalimbali.  Kutoka kushoto ni Mwanasheria Mwandamizi wa Serikali mkoani Bukoba, Sakina Husein Sinda,Mganga Mkuu wa Halmsahauri ya Wilaya ya Bukoba, Hamza Mugura, Mkurugenzi wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya inayofanya shughuli zake mjini Bukoba ya KADETFU, Yusto Muchuruza, Mshauri wa Fr.James, Enic Kashasha na Andrew Kailembo, Mmiliki wa Walkgard Hoteli, Adventina Matungwa na Dk.Julius Zelothe.

 Wanahabari wakiwa kwenye promosheni hiyo.
 Wadau wakiwa kwenye promosheni hiyo
Promosheni imenogaaaa.
 Wadau wakiwa kwenye promosheni hiyo.
 Mkurugenzi wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya inayofanya shughuli zake mjini Bukoba ya KADETFU, Yusto Muchuruza,akichangia mada katika promosheni hiyo.
Hapa Windhoe imependezaaa ni tamuuuuuuu
 Wadau wakipata kinywaji cha Windhoek katika promosheni hiyo.



Thursday, November 6, 2014

FR JAMES RUGEMALIRA AHIMIZA UWEKEZAJI MKOANI KAGERA


 Katibu Mkuu mstaafu wa Shirikisho la vyama huru vya wafanyakazi (ICFTU/AFRO), Andrew Kailembo(kulia), akiwa katika mkutano wa wadau mbalimbali wa kujadili maendeleo ya mkoa wa Kagera uliofanyika jana.

 Wakili wa Kujitegemea, wa IMMMA ADVOCATES, Protas Ishengoma akiongoza mkutano huo.


 REV.Fr Kamugisha (kulia), ambaye ni Mkurugenzi wa Hoteli ya Kolping akichangia mada. Kutoka kushoto ni Mshauri wa Kimataifa wa Kujitegemea, Fr, James Rugemalira na Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali mstaafu, Fabian Masawe.
 Wanahabari wa mkoa wa Kagera wakiwa kwenye mkutano huo.
Mkuu wa Utawala wa Jumuia ya Afrika Mashariki, mstaafu, Abdul Katabaro naye alipata fursa ya kuchangia katika mkutano huo muhimu wa kuhimiza uwekezaji mkoani humo.

Wednesday, November 5, 2014

MAMIA WAJITOKEZA KUMZIKA KWA HESHIMA KUBWA MKE WA JAJI JOHN RUHANGISA ALIYEFARIKI KWA AJALI YA GARI JIJINI ARUSHA

 Mke wa Jaji John Ruhangisa, Marehemu Laetitia 
Kokuhangisa Ruhangisa enzi za uhai wake.
 Jaji John Ruhangisa
 Jaji John Ruhangisa (wa pili kushoto), akiwa na watoto wake wakati wa ibada ya mazishi ya mke wake Laetitia Kokuhangisa Ruhangisa iliyofanyika nyumbani kwake katika Kijiji cha Ibwera mkoani Kagera leo jioni. Kutoka kulia ni mtoto wake wa kwanza Moreen, David na Fiona.
 Mapadre 30 wa Kanisa Katoliki wakiwa kwenye ibada 
hiyo ya mazishi.
 Viongozi mbalimbali , majaji, watawa na wananchi 
wakiwa kwenye ibada hiyo.
 Watawa wakiwa kwenye ibada hiyo.
 Waimbaji wa Kwaya ya Kanisa Katoliki Parokia ya Ibwera 
nao walikuwepo kwenye ibada hiyo.
 Watoto wa Kanisa Katoliki wanaoshiriki kuongoza ibada mbalimbali wakiwa kwenye ibada hiyo.
 Watoto wa Kijiji cha Ibwera nao walijumuika katika 
mazishi ya mama yao Kokuhengesa.
 Jaji John Ruhangisa akimfariji mtoto wake David.
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Bukoba, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Henry Mwaibambe akimpa pole  mtoto wa marehemu, David John Ruhangisa.
 Hii ndio nyumba ya milele ya  mpendwa wetu  mke wa Jaji John Ruhangisa, Marehemu Laetitia Kokuhangisa Ruhangisa alimo lala nje ya nyumba Kijijini Ibwera. Bwana alitoa na bwana ametwaa jina lake libarikiwe.
 Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa marehemu, Laetitia Kokuhangisa Ruhangisa wakielekea kaburini tayari kwa mazishi.
 Jeneza likishushwa kaburini.

 Jaji John Ruhangisa akiweka udongo kaburini wakati wa 
mazishi ya mke wake. Kushoto ni shemeji yake Sizer.
 Padre aliyeongoza ibada hiyo akiweka msalaba katika kaburi la Laetitia Kokuhangisa Ruhangisa.
 Jaji John Ruhangisa akifarijiana na watoto wake aliowakumbatia, Moreen (kulia) na Fiona (kushoto. Hakika inahuzunisha.
 Jaji John Ruhangisa na watoto wake wakiweka shada 
la maua kaburini.
 Mshauri wa Kimataifa wa Kujitegemea, Fr. James Rugemalira akisaini katika  kitabu cha maombelezo.
 Mdau Erick Kashasha naye alikuwa ni miongoni mwa waombolezaji waliosaini katika kitabu cha maombolezo.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Bukoba akisaini katika kitabu cha maombolezo.(Imeandaliwa na mtandao a www. habari za jamii.com)


Dotto Mwaibale

SIMANZI na majonzi viligubika leo jioni  katika mazishi ya mke wa Jaji John Ruhangisa, Marehemu Laetitia Kokuhangisa Ruhangisa aliyefariki kwa ajali ya gari jijini Arusha.

Mazishi hayo yaliyofanyika katika Kijiji cha Ibwera katika mkoani Bukoba.

Viongozi  mbalimbali wa Serikali na vyama vya siasa, Majaji, dini na wageni waalikwa kutoka ndani na nje ya mkoa wa Bukoba walikuwa ni miongoni mwa watu waliohudhuria mazishi hayo.

Akizungumza katika mazishi hayo Rais wa Mahakama ya Afrika Mashariki, Dk. Emmanuel Ugirashebuja alisema kifo cha mke wa Jaji Ruhangisa kiliwashitua na kuwahunisha.

"Kifo cha mke wa mwenzetu kimetusikitisha sana kwani marehemu enzi za uhai wake tulikuwa tukijumuika naye kwa mambo mbalimbali kwa kweli tupepoteza mtu muhimu" alisema 

Ugirashebuja alisema mafanikio yote aliyoanyo Jaji John Ruhangisa yametokana na maisha ya upendo aliyokuwa mke wake kwake ndio maana alipata fursa ya kufanya kazi kwa bidii kwa kuwa hakuwa na matatizo nyumbani kwake.

Mazishi hayo yalihudhuriwa na majaji kadhaa akiwemo Rais aliyepita wa  Mahakama ya Afrika Mashariki, Jaji Nsekela, Jaji Rutakangwa aliye mwakilisha Jaji Mkuu wa Tanzania, Mwakilishi kutoka Halmshauri ya Meru

Mke wa Jaji Ruhangisa alipoteza maisha Oktoba 29 mwaka huu  Tengeru mkoani Arusha wakati akitoka kazini baada ya Hiace aliyokuwa amepanda kugongwa na lori la mafuta.

Katika ajali hiyo watu 12 walipoteza maisha wakiwemo maofisa elimu watatu wa Halmshauri ya Meru