Tuesday, March 25, 2014

TBS YAWAFUNDA WALEMAVU WASIOSIKIA (VIZIWI) KUTOKA MIKOA YA DODOMA,SINGIDA, TABORA NA SHINYANGA JUU YA UZALISHAJI WA BIDHAA KWA KUZINGATIA VIWANGO VYA UBORA

Meza kuu ikiongozwa na Mkuu wa mkoa Dodoma Dr. Rehema Nchimbi wakiwashangilia kwa lugha ya alama wajasiriamali wenye ulemavu wa kusikia (hawapo pichani) wakati wakijitambulisha kwenye semina iliyoandaliwa na TBS kwa ajili ya kuwafunda walemavu hao masuala ya viwango vya ubora  katika shughuli za,uzalishaji  iliyofanyika mapema Leo hii.
Mkuu wa mkoa Dodoma Dr Rehema Nchimbi akiwasisitizia walemavu wasiosikia (viziwi) kuzingatia ubora wa viwango kwenye bidhaa wanazozalisha kwenye sekta ya kilimo, ufugaji nyuki na mifugo na ujasiriamali ili kunufaika na masoko ya kimataifa wakati akifungua semina kwa walemavu hao juu ya masuala ya ubora wa viwango  iliyoandaliwa na shirika la viwango tanzania TBS, semina hiyo ilifanyika leo mjini Dodoma, wengine pichani ni maafisa kutoka TBS.
Baadhi ya wajasiriamali wenye ulemavu wa kusikia (viziwi) wanaojihusisha na shughuli za uzalishaji katika sekta za kilimo, ufugaji mifugo na nyuki na ujasiriamali kutoka mikoa ya Dodoma, singida, Tabora na shinyanga wakishangilia hotuba ya ufunguzi iliyotolewa na mkuu wa mkoa Dodoma na kutafsiriwa kwa lugha ya alama kwenye semina ya masuala ya ubora wa viwango iliyoandaliwa na shirika la viwango tanzania TBS mapema Leo mjini Dodoma.
Picha ya pamoja baina ya mkuu wa mkoa wa dodoma Dr. Rehema Nchimbi, wataalamu wa masuala ya viwango vya ubora kutoka TBS na walemavu wasiosikia (viziwi) kutoka mikoa ya Dodoma, Singida, Tabora na shinyanga muda mfupi baada ya mkuu huyo wa mkoa kufungua semina kwa walemavu hao juu ya  masuala ya ubora wa viwango iliyoandaliwa na shirika la viwango tanzania TBS na kufanyika mapema Leo Jumatatu Machi 24, 2014.


PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI ZA KILELE CHA MAADHIMISHO YA WIKI YA MAJI MKOANI DODOMA.


Waziri Mkuu mizengo pinda akisalimiana na viongozi wa serikali na viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama mkoa Dodoma muda mfupi mara baada ya kuwasili kwenye viwanja vya jamhuri mjini Dodoma kuhitimisha maadhimisho ya wiki ya maji kitaifa mkoani dodoma machi 22.
Teknolojia rahisi ya uvunaji maji ya mvua kwenye majengo/makazi yetu ni moja kati ya elimu iliyowavutia wananchi wengi wakati wote wa maadhimisho ya wiki ya maji kitaifa mkoani dodoma yaliyoambatana na maonesho ya huduma za maji kwenye viwanja vya jamhuri mjini Dodoma kuanzia machi 16 had 22, 2014.

 Baadhi ya maafisa wa ngazi za juu wa baadhi ya  vyombo vya ulinzi na usalama mkoa Dodoma wakipata ufafanuzi juu ya pampu za kuvuta na kusukuma maji; elimu juu ya vifaa vya ujenzi wa miundombinu ya maji, uhifadhi na utunzaji vyanzo na rasilimali za maji zilitolewa kwa wingi kwenye maadhimisho hayo yaliyoambatana na maonesho ya huduma za maji kwenye viwanja vya jamhuri mjini Dodoma.