Friday, February 28, 2014

MAMBO YA BUNGE MAALUM LA KATIBA MJI WA DODOMA KWA SASA MAGARI KUONGOZWA NA TAA ZA BARA BARANI.

Mafundi wa kampuni ya Makenga Invest LTD ya moani Tabora wakifunga taa kwa ajili ya kuongozea madereva wanaendesha vyombo mbalimbali vya
barabarani mjini Dodoma, kwa mujibu wa kampuni hiyo taa hizi zinafungwa
maeneo ya njiapanda ya Area D, na Ndasha.

PICHA NA JOHN BANDA

Sunday, February 23, 2014

MKANDARASI MATATANI KWA KUJENGA BARABARA KWA KIWANGO CHA CHINI DODOMA.


Gari likionekana kujarib kupita bila mafanikio  katika barabara
inayonganisha vijiji sita vya wilaya ya Bahi, adha hiyo ya usafiri
imetokana na kujengwa kwa kutumia udongo mifinyanzi katika kijiji cha
Tobai.

Shimo lililochimbwa na kikata barabra ya Lukali kongogo  kwa
ajili ya kutengenea karavati bila kuwa na njia mbadala hali
iliyosababisha adha kubwa kwa usafiri  huku mkandarasi wa ujenzi wa
huo akijiojitetea kutosubili ili kukwepa hasara kwa kampni yake.

Gari la mizigo likiwa limekwama katika barabara hiyo
inayojengewa karavati kwa kufungwa bila kuweka njia mbadala kwa ajili ya
safiri kutokana njia kuwa moja na kutumika na wananchi wa vijiji zaidi
ya sita huku mhandisi wa Wilaya ya Bahi Josephu Mkinga akiifunga kwa
masaa 48 ili kupisha ujenzi huo.

Tuesday, February 18, 2014

LOWASA,MEMBE,WASIRA NA NGELEJA WAPEWA ONYO KALI NA KAMATI YA MAADILI YA CCM.

KAMATI YA MAADILI CCM 

 TAARIFA RASMI YA CCM
Kati ya tarehe 13/02/2014  na tarehe 18/02/2014 kumekuwa na mfululizo wa vikao kadhaa vya Chama kitaifa vilivyoshughulikia suala la maadili ndani ya Chama.

Vikao hivyo ni pamoja na Kamati Ndogo ya Udhibiti tarehe 13-14/02/2014, Tume ya Udhibiti na Nidhamu 18/02/2014 na Kamati Kuu tarehe 18/02/2013.

Waliohojiwa katika mfululizo wa vikao hivi ni wafuatao:-

     1.    Ndgugu Frederick Sumaye
2.    Ndugu Edward Lowasa
 3.    Ndugu Bernard Membe 
4.    Ndugu Stephen Wassira
      5.    Ndugu January Makamba  
6.    Ndugu William Ngeleja

Baada ya kuwahoji ilithibitika kuwa baadhi ya tuhuma dhidi yao ni za kweli na hivyo kupendekeza adhabu.  Mapendekezo hayo yalipelekwa kwenye Tume ya Udhibiti na Nidhamu na hatimaye Kamati Kuu ya CCM ambayo ilitoa adhabu kwa wahusika.

Kwa ujumla waliohojiwa wamethibitika kuwa na makosa yafuatayo:-

1.    Walithibitika kuanza kampeni za kutafuta kuteuliwa kugombea Urais kabla ya wakati kinyume na Kanuni za Uongozi na Maadili za CCM Toleo la Februari 2010, Ibara 6(7)(i).

2.    Wamethibitika kufanya vitendo vinavyokiuka maadili ndani ya Chama na baadhi yao kufanya vitendo vinavyokiuka maadili ndani ya jamii.  Kosa hili nalo ni kwa mujibu wa Kanuni za Uongozi na Maadili za CCM Toleo la Februari 2010, Ibara kadhaa za kanuni hizo.

Kamati Kuu baada ya kuthibitisha makosa hayo imewapa watu wote sita waliohojiwa adhabu ya ONYO KALI na kuwataka wajiepushe na vitendo vinavyokiuka maadili na iwapo wataendelea na vitendo hivyo Chama kitawachukulia hatua kali zaidi.

Tafsiri ya adhabu ya ONYO KALI kwa mujibu wa Kanuni za Uongozi na Maadili za CCM Toleo la Februari 2010, Ibara ya 8(ii) (b) ni:-

“Mwanachama aliyepewa adhabu ya ONYO KALI atakuwa katika hali ya kuchunguzwa kwa muda usiopungua miezi 12, ili kumsaidia katika jitihada zake za kujirekebisha.”

Kamati Kuu imeitaka pia Kamati Ndogo ya Udhibiti kuwachunguza na kuchukua hatua kwa wote waliohusika kwa namna moja au nyingine (mawakala na wapambe) kufanyika kwa vitendo hivyo vilivyovunja Kanuni za Chama.

Aidha, Kamati Kuu imewaonya vikali Viongozi na Watendaji wa Chama na kuwataka kujiepusha kujihusisha na matendo ya wanawania Urais yanayovunja na kukiuka maadili ya Chama, wametakiwa kuzingatia Kanuni na taratibu za Chama.

Imetolewa na:- 
Nape Moses Nnauye,
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA,
ITIKADI NA UENEZI,
18/02/2014
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
KAMATI YA MAADILI CCM

                                 TAARIFA RASMI YA CCM KWA VYOMBO VYA HABARI.

Kati ya tarehe 13/02/2014 na tarehe 18/02/2014 kumekuwa na mfululizo wa vikao kadhaa vya Chama kitaifa vilivyoshughulikia suala la maadili ndani ya Chama.

Vikao hivyo ni pamoja na Kamati Ndogo ya Udhibiti tarehe 13-14/02/2014, Tume ya Udhibiti na Nidhamu 18/02/2014 na Kamati Kuu tarehe 18/02/2013.

Waliohojiwa katika mfululizo wa vikao hivi ni wafuatao:-

1. Ndgugu Frederick Sumaye
2. Ndugu Edward Lowasa
3. Ndugu Bernard Membe
4. Ndugu Stephen Wassira
5. Ndugu January Makamba
6. Ndugu William Ngeleja

Baada ya kuwahoji ilithibitika kuwa baadhi ya tuhuma dhidi yao ni za kweli na hivyo kupendekeza adhabu. Mapendekezo hayo yalipelekwa kwenye Tume ya Udhibiti na Nidhamu na hatimaye Kamati Kuu ya CCM ambayo ilitoa adhabu kwa wahusika.

Kwa ujumla waliohojiwa wamethibitika kuwa na makosa yafuatayo:-

1. Walithibitika kuanza kampeni za kutafuta kuteuliwa kugombea Urais kabla ya wakati kinyume na Kanuni za Uongozi na Maadili za CCM Toleo la Februari 2010, Ibara 6(7)(i).

2. Wamethibitika kufanya vitendo vinavyokiuka maadili ndani ya Chama na baadhi yao kufanya vitendo vinavyokiuka maadili ndani ya jamii. Kosa hili nalo ni kwa mujibu wa Kanuni za Uongozi na Maadili za CCM Toleo la Februari 2010, Ibara kadhaa za kanuni hizo.

Kamati Kuu baada ya kuthibitisha makosa hayo imewapa watu wote sita waliohojiwa adhabu ya ONYO KALI na kuwataka wajiepushe na vitendo vinavyokiuka maadili na iwapo wataendelea na vitendo hivyo Chama kitawachukulia hatua kali zaidi.

Tafsiri ya adhabu ya ONYO KALI kwa mujibu wa Kanuni za Uongozi na Maadili za CCM Toleo la Februari 2010, Ibara ya 8(ii) (b) ni:-

“Mwanachama aliyepewa adhabu ya ONYO KALI atakuwa katika hali ya kuchunguzwa kwa muda usiopungua miezi 12, ili kumsaidia katika jitihada zake za kujirekebisha.”

Kamati Kuu imeitaka pia Kamati Ndogo ya Udhibiti kuwachunguza na kuchukua hatua kwa wote waliohusika kwa namna moja au nyingine (mawakala na wapambe) kufanyika kwa vitendo hivyo vilivyovunja Kanuni za Chama.

Aidha, Kamati Kuu imewaonya vikali Viongozi na Watendaji wa Chama na kuwataka kujiepusha kujihusisha na matendo ya wanawania Urais yanayovunja na kukiuka maadili ya Chama, wametakiwa kuzingatia Kanuni na taratibu za Chama.

Imetolewa na:-
Nape Moses Nnauye,
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA,
ITIKADI NA UENEZI,
18/02/2014

Monday, February 17, 2014

CCM WATANGAZA RASMI NI WAUMI WA SERIKALI MBILI.


 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa Habari nje ya ukumbi wa NEC mjini Dodoma ambapo aliwaeleza kuwa Kikao cha NEC kilikamilika vizuri ambapo wajumbe waliijadili Rasimu vizuri na CCM kubaki na msimamo wa Serikali mbili .
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa Habari nje ya ukumbi wa NEC mjini Dodoma na kuwaambia CCM bado imebaki na msimamo wake wa muundo Serikali mbili wenye maboresho.

Sunday, February 16, 2014

UONGOZI WA UDOM WALALAMIKIWA NA WAENDESHA BODABODA KWA KUWAPIGA MARUFUKU KUFANYA BIASHARA HIYO KATIIKA ENEO LA CHUO.


Mmoja wa viongozi wa waendesha Bodaboda wanao toa huduma ya usafiri
ndani na n je ya chuo hicho  akiwagawia funguo za pikipiki zao baada
ya jana kutotoa huduma hiyo kwa zaidi ya saa 7 wakijadili nini cha
kufanya baada ya kutakiwa kutopakilia abiria katika kituo hicho
kilichopo chuo cha elimu ndani ya UDOM Dodoma.

Madereva wa Bodaboda wakiwa wamekusanyika pamoja wakijadiliana jambo wakati wakifikili nini cha kufanya baada ya kuona askari walinzi wa
chuo kikuu cha Dodoma [ UDOM]  Kuwafukuza na kuwataka kutopakilia
Abiria katika kituo hicho kilichopo katika majengo ya mchepuo wa
elimu.

Waendesha pikipiki za kusafirishia abiria maarufu kama Bodaboda wakuwa
wameziegesha  katika kituo cha Daladala cha maktaba ya ualimu
kilichopo Chuo kikuu kikuu cha Dodoma [UDO], madereva hao
wamelalamikia kunyanyaswa na walinzi chuoni hapo kwa kukamatwa na
kutishiwa kuvunjwa miguu bila sababu za kueleweka.