Thursday, January 31, 2013

JK-Tunajua biashara ya dini inalipa, lakini msiivuruge Tanzania




“Kuna baadhi ya watu wanatumia vigezo vya kidini kwa ajili ya kufanya vurugu za kuhatarisha amani, Serikali haitaweza kuwavumilia, badala yake tutatumia njia mbalimbali RAIS Jakaya Kikwete amesema kuwa mtindo wa kufanya fujo na kusababisha uvunjifu wa amani kwa visingizio vya dini nchini ni biashara inayolipa na ndiyo maana...

Mafuta Yakigunduliwa Tarime ITAKUWAJE...?

kp31012013 27679

Na Mtindo Huu Wa Nywele Unaitwaje?

7 20d32

Makubwa Haya; " Haya, Nani Anauzika Sokoni?!"

5 79f23
Nimeyakuta Kisolanza, Mufindi, hivi karibuni. Ama, tembea ujionee!

MAMBO YA KANGA MOKO HAYOOOOO.



Mmmhhh... uchezaji gani huu jamani? Ndo mambo ya akina 'Khanga Moko Laki Si Pesa, Milioni Moja Paketi Money'
Tobaaa....! Namna hii tutasalimika kweli? Huyu naye ni memba wa walewale akina 'Kitu T' na 'Kanga Moko'

WANANCHI WA WILAYA YA KILWA LINDI, WAANZA KUNUFAIKA NA MRADI WA GESI ASILIA


Mkuu wa wilaya ya Kilwa Abdallah Ulega, (kushoto) akishuhudia zoezi la utiaji wa sahihi wa mkataba huo wa miaka mitatu kati ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kilwa, Addo Mapunda akitiliana saini na  Mratibu wa Mradi wa mpango wa ufundishwaji wa Lugha ya Kingereza kwa njia ya teknorojia ya kisasa (Techonoroji Enhanced Edcation) TEE-TZ chini ya ufadhili wa kampuni ya Pan African Energy,inayojishughulisha na kazi ya uchimbaji,usambazaji na uuzaji wa gesi asilia ya Songosongo Bi Anne Devilliers, wakati wa hafla hiyo fupi ya kutiliana saini iliyofanyika leo.

Makabidhiano

RAIS KIKWETE AFANYA MAZUNGUMZO NA RAIS KABILA IKULU, AMSINDIKIZA MGENI WAKE LEO

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mgeni wake Rais Joseph Kabila Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kabla ya kufanya naye mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam jana jioni.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsidikiza  Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), wakati akiondoka Ikulu Dar es Salaam, jana.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsidikiza  Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere baada ya kufanya naye mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam jioni hii ya Januari 30. 2013. PICHA NA IKULU

ZIARA YA KINANA WILAYANI KAKONKO MKOANI KIGOMA

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akikagua ujenzi wa daraja la Umoja linalounganisha Kata ya Nyabibuye, Kakonko na vijiji jirani vya Burundi. alipokuwa katika ziara wilayani Kakonko mkoani Kigoma, Januari 30, mwaka huu, ikiwa ni sehemu ya ziara ya Katibu Mkuu inayoambana na maadhimisho ya miaka 36 ya CCM ambayo kilele chake ni Februari 3, mwaka huu mjini Kigoma.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akikagua soko la Kata ya Nyabibuye, Kakonko leo Januari 30, 2013, ikiwa ni ziara ya Katibu Mkuu inayoambana na maadhimisho ya miaka 36 ya CCM ambayo kilele chake ni Februari 3, mwaka huu mjini Kigoma. Kushoto ni diwani wa kata hiyo Steven Mnigakiko na kulia ni Mkuu wa wilaya ya Kakonko Peter Toima.
  Wananchi wa rika zote wa Kijiji cha Rumashi, Kata ya Nyabibuye, wilayani Kakonko, Kigoma wakimshangilia Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahma Kinana kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika leo, Januari 30, 2013,katika  kijiji hicho, ikiwa ni sehemu ya ziara ya Katibu Mkuu inayoambana na maadhimisho ya miaka 36 ya CCM ambayo kilele chake ni Februari 3, mwaka huu mjini Kigoma.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Rumashi, Kata ya Nyabibuye, wilaya ya Kakonko mkoani  Kigoma, ikiwa ni sehemu ya ziara ya Katibu Mkuu inayoambana na maadhimisho ya miaka 36 ya CCM ambayo kilele chake ni Februari 3, mwaka huu mjini Kigoma.
 Kinana akiwasalimia wanafunzi wa shule hiyo ya Nyamtukuza wilayani Kakonko mkoani Kigoma, akiwa katika ziara ambayo ni sehemu ya ziara ya Katibu Mkuu inayoambana na maadhimisho ya miaka 36 ya CCM ambayo kilele chake ni Februari 3, mwaka huu mjini Kigoma. Kulia ni Mkuu wa shule hiyo Amani Ntibakiza.
 Kinana akizungumza na wanafunzi wa shule hiyo ya Nyamtukuza wilayani Kakonko mkoani Kigoma, akiwa katika ziara ambayo ni sehemu ya ziara ya Katibu Mkuu inayoambana na maadhimisho ya miaka 36 ya CCM ambayo kilele chake ni Februari 3, mwaka huu mjini Kigoma.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa shule ya sekondari ya Nyamtukuza wilayani Kakonko mkoa wa Kigoma,  akiwa katika ziara ambayo ni sehemu ya ziara ya Katibu Mkuu inayoambana na maadhimisho ya miaka 36 ya CCM ambayo kilele chake ni Februari 3, mwaka huu mjini Kigoma.
 Daraja la Umoja linalojengwa kuunganisha Kata ya Nyabibuye, Kakonko Tanzania na mkoa wa Changuzo Burundi.

KUTOKA BUNGENI MJINI DODOMA JANA, PINDA AWATAKA WANAMTWARA KUWA WATULIVU

 Waziri Mkuu Mizengo Pinda (kulia)  akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma jana, ambapo alieleza  taarifa mbalimbali kuhusu ziara yake  Mkoani  Mtwara kuhusu kusikiliza maoni ya wananchi wa Mtwara katika sakata la gesi. Waziri Mkuu amewaomba Viongozi wa Mkoa huo kuwashirikisha wananchi katika mambo mbalimbali. Aidha amewaomba wana Mtwara kuwa watulivu na amewahakikishia usalama na amani itaendeelea kupatikana mkoani hapo (kulia) ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt. Emmanuel Nchimbi.
 Naibu Waziri wa  Nishati na Madini, George Simbachawene, akijibu hoja mballimbali za Wizara yake leo Bungeni mjini Dodoma.
 Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni Freeman Mbowe (kulia) , Godless Lema (katikati- Aruha mjini) pamoja na Moses Machali (NCCR- Mageuzi- kulia) wakielekean katika ndani ya Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma leo. Mbunge  Lema amerudi tena Bungeni  baada ya kushinda kesi yake.
 Baadhi ya wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakielekea ndani ya ukumbi wa Bunge leo mjini Dodoma.
Wabunge wa Iramba  Magharibi Mwingulu Nchemba(kulia),Joseph Selasini( wa Rombo akiwa katikati), na Mbunge wa NCCR- MAGEUZI, Moses Machali wakiwa katika viwanja vya Bunge leo mjini Dodoma. Picha na Mwanakombo Jumaa- MAELEZO

Monday, January 28, 2013

mh.lowassa anusurika ajalini

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli na Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama Edward Lowassa
 Gari la  Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli na Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama Edward Lowassa likiwa limebonyea kwa ubavuni baada ya kupata ajali iliyotokea leo asubuhi

bongo movies walivyoiteka dar live


Mrembo Jacqueline Wolper akiwapa ‘hi’ mashabiki.
Jacob Steven ‘JB’ akionyesha umahiri wake wa kusakata rhumba wakati wa tamasha hilo.

KINANA NA MSAFARA WAKE WAKAGUA MATENGENEZO YA UWANJA WA NDEGE WA KIGOMA


Msafara wa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na ujumbe wake, ukiingiwa kwenye eneo la Uwanja wa Ndege wa Kigoma uliopo eneo la Kipampa, kwa ajili ya kushuhudia maendeleo yaliyofikiwa katika ujenzi mkubwa wa kiwanja hicho unaoendelea ili kukiongezea uwezo.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwasalimia wafanyakazi kwenye uwanja huo alipowasili.
Meneja wa Uwanja huo, Elipind Tesha (kulia) akimweleza  Kinana na ujumbe wake hatua ilipofikiwa katika ujenzi huu, ambapo alisema, umefikia asilimia tisini, na kwamba unaweza ingawa unaweza kuanza kutumika rasmi Aprili mwaka huu, lakini matengenezo yote yatakuwa yamekamilika Juni 2013. Wengine kutoka kushgoto ni, Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro, Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM, Martin Shigela.
Kinana akimsikilliza Mhandisi Mkazi wa Uwanja huo,Cleopa Mpembeni (wapili kulia) akimpa maelezo ya kiufundi kuhusu ujenzi unavyoendelea.

Wenye nyumba za kupangisha kaeni tayari kulipa kodi!

 UONGOZI wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), wamesema wanakuna vichwa juu ya  jinsi ambavyo watafanikisha kukusanya kodi kutoka kwa wenye nyumba nchini wanaofanya biashara ya kuzipangisha.

Kamishna Mkuu wa TRA, Harry Kitillya alisema jijini hapa mwishoni mwa wiki kwamba kuna changamoto nyingi katika ukusanyaji wa kodi kutoka kwenye nyumba zilizopangishwa.

Alisema ni kawaida kwa kila mtu anayepata fedha kihalali lazima alipe kodi, lakini utaratibu wa kudai kodi kutoka kwenye nyumba zilizopangishwa bado unatafutwa.

“Katika ukusanyaji wa kodi changamoto ipo kwenye kukusanya kodi inayotokana na biashara ya upangisaji, kwa sababu wenye nyumba wengine hawataki kuonyesha mikataba halisi, lakini sasa tumepata wazo tofauti ambalo tunalifanyia kazi ni kutafiti kwamba bei za nyumba za kupanga kulingana na eneo husika, mfano tukijua Masaki wanapangisha nyumba kwa kiasi gani tutakuwa tumepata pa kuanzia, pia tunataka kulifanya suala hili kwa kuhakikisha sheria inatumika ipasavyo,” alisema Kitillya

LULU APEWA DHAMANA, JE KWA SASA KUWA NJE NI SALAMA?



Mahakama Kuu ya Tanzania,  imemwachia kwa dhamama msanii Elizabeth Michael 'Lulu', aliyekuwa akikabiliwa na kesi ya kudaiwa kuuwa bila kukusudia,  msanii mwenzake Steven Kanumba, mwaka jana.


Lulu amepewa dhamana hiyo baada ya Makama kupitia vifungu kadhaa na kuona kesi yake ya kuua bila kukusudia inamruhusu kupewa dhamana.

Msanii huyo ambaye anatuhumiwa kuhusika na kifo cha msanii mwenzake, Steven Kanumba - The Great, alibadilishiwa kosa la kuua na kuwa kuua bila kukusidia, ambalo, kwa mujibu wa sheria linadhamnika na kwamba ikiwa mtuhumiwa atapatikana na hatia, adhabu ya juu kabisa ni kifungo cha maisha, miaka kadhaa au kuachiwa huru
Msanii Lulu wakati akiwa Mahakamani leo asubuhi alipokuwa akisomewa taratibu za dhamana yake, ambapo kwa upande wa Mawakili wa Serikali walisema kuwa hawana pingamizi na dhamana hiyo.

Ikumbukwe kuwa Msanii huyo aliwahi kuomba ruhusa ya kuhudhuria mazishi ya rafikie kipenzi, Steven Kanumba, kwenye mazishi yake, wakati alipokuwa rumande, lakini kwa kuhofia usalama wake vyombo husika viligoma na kuelezea kuwa usalama wake utakuwa hatarini.

Sasa je kwa kupewa dhamana msanii huyo hivi sasa ataweza kuishi kwa amani mtaani kama alivyozoea? na je atahakikishiwa usalama wake popote aendako? na vipi familia yake imejiandaaje kumlinda kwa kipindi hiki atakapokuwa nje kwa dhamana? hayo ni miongoni mwa maswali yanayotawala vichwani kwa wanaoliangala jambo hili kwa jicho la tatu.

Inaaminika wananchi walio wengi, mashabiki wake na wengineo wana hamu sana ya kumuona akiwa nje na walikuwa wakimuonea huruma sana msanii huyo kwa kile kilichomkuta, lakini kwa sasa ni jukumu la kila mmoja wetu aliye karibu na msanii huyu, na hata kila mmoja kwa wakati wake kumlinda msanii huyu kwa njia yeyote ile ili asijekutimia ile sehemu ya maneno yake wakati akiwa rumande, kwa kufanya lolote kwa kuogopa maneno ya wanajamii.

KUMBE DR ULIMBOKA SHABIKI WA YANGAAAAAAAAAAAA

 Mashabiki wa Yanga, wakishangilia bao la Mbuyu Twite.
 Dkt. Steven Ulimboka, akijumuika na mashabiki wenzake wa Yanga jukwaani, wakati wa mchezo huo.

YANGA YAZIDI KUONYESHA VITU VYA UTURUKI, YAICHAPA TZ PRISONS 3-1

 Mshambuliaji wa Yanga, Jerry Tegete, 'Mkali wa Uturuki', akishangilia bao lake la pili, huku kipa wa Tanzania Prisons, akishangaa akiwa chini baada ya kushindwa kuokoa mpira huo uliopigwa na mkali huyo wa Uturuki. katika dakika ya 82. ambapo bao la kwanza pia lilifungwa na mkali huyo na la pili lilifungwa na Mbuyu Twite. Hadi mwisho wa mchezo huo Yanga 3-Tanzania Prisons 1.
 Simon Msuva, akipiga krosi, wakati wa mchezo huo wa fungua dimba ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara, mzunguko wa pili kwa upande wa timu hizo, uliochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar Es Salaam.
 Didier Kavimbangu, akijaribu kutupia, wakati wa mchezo huo, ambapo shuti hilo lilipaa juu ya goli.
 Sehemu ya mashabiki wa Yanga, wakishangilia bao la tatu lililoizamisha Tanzania Prisons na kuvunja matumaini ya kusawazisha na kuwafanya wachezaji wa Prisons, kuanguka kila mara ambapo kila aliyekuwa akianguka alikuwa ameshikwa na msuli.

Friday, January 25, 2013

SIMBA YA OMAN YAIOGOPA BLACK LEOPARD YAINGIZA KIKOSI CHA PILI NA KUPOKEA KIPIGO KIKALI

Baada ya kipigo cha mara mbili mfululizo kutoka kwa timu ya Yanga ya jijini Dar es Salaam, timu ya Black Leopards ya nchini Afrika ya Kusini, leo imepunguza machungu yake kwa kuichapa Simba ya jijini Dar es Salaam kwa bao 1-0, katika mchezo wao wa kirafiki wa kimataifa uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. 

Hata hivyo imeelezwa kuwa kutokana na hofu Klabu ya Simba iliwachezesha wachezaji wa timu B, jambo ambalo limewakera hadi mashabiki wa Simba waliokuwapo uwanjani hapo leo, ambapo baadhi ya mashabiki waliohudhuria mtanange huo uwanjani hapo walisikika wakilalama kwa kitendo hicho, ambacho kimeelezwa kuwa ni sehemu ya hofu na dharau.

Katika Kikosi cha simba wameonekana wachezaji wanne tu walio katika kikosi cha kwanza cha ligi kuu. huku wachezaji wote waliobaki wakiwa ni wa kikosi cha pili, ambao wengi wao wakiwa ni watoto

CHEKI MH RAIS KIKWETE AKIWA NA SEPP BLATTER MAKAO MAKUU YA FIFA ZURICH

Zurich Switzerland.
.
Sepp Blatter rais wa Fifa akiwa na President Kikwete na Leodgar Tenga rais wa TFF.
.
.
Picha zimepigwa na Fred Maro wa Ikulu

Thursday, January 24, 2013

HIII NDIO YANGAAAAAAAAAAA



 
Golikipa wa timu ya Black Leopards, Posnett Omony, akisota kuokoa mpira uliotinga wavuni kutoka kwa mchezaji wa timu ya Yanga, Jerry Tegete, kwa njia ya penati.Timu ya Yanga imeibuka kidedea kwa kuinyuka Black Leopards mabao 2-1 katika mchezo wa marudiano wa kimataifa wa kirafiki uliochezwa leo jioni kwenye Uwaja wa CCM Kirumba. Bao la kwanza la Yanga lilifungwa na Said Bahanuzi.
 Wachezaji wa timu Yanga wakishangilia bao la pili lililofungwa na Jerry Tegete, katika  kipindi cha pili kwa mkwaju wa penati.
Mchezaji wa wa timu ya Yanga David Luhende (kulia) akipiga krosi huku Moses Kwena wa Black Leopards, akijaribu  kumdhibito wakatia wa mchezo huo uliochezwa leo jioni kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
 Pichani ni Golikipa wa Black Leopards Posnett Omony akijitahidi kuokoa mpira uliopigwa kwa kichwa na mchezaji wa Yanga,Said Bahanuzi na hatimaye kutinga kimiani na kuandika bao la kwanza.

USIKU WA TARANGIRE WAFANA VILIVYO

Wanamuziki wa Bendi ya FM Academia wakionesha vitu vyao wakati wa Hafla ya usiku wa Tarangire iliyofanyika kwenye hifadhi hiyo ya Taifa.
Mkuu wa Mkoa Dodoma Dr. Rehema Nchimbi (mwenye kilemba/miwani), Mkuu wa Mkoa Manyara Elaston Mbwilo (kulia kwa Dr. Nchimbi) Uongozi na wafanyakazi wa Hifadhi ya Taifa Tarangire wakiserebuka kwa muziki wa Bendi ya FM Academia wakati wa hafla ya Usiku wa Tarangire iliyofanyika hifadhini hapo
Mwanamuziki wa Bendi ya FM Academia Nyoshi El – Saadat (katikati) akifungua Champaign kwenye hafla ya Usiku wa Tarangire iliyofanyika hifadhini hapo ambapo Bendi hiyo FM Academia ilitumbuiza na pia iliimba kibao maalumu kinachohamasisha utalii wa ndani kwa watanzania.