Wednesday, November 20, 2013

MKUU WA MKOA DODOMA AWAONGOZA MAMIA YA WANAJUMUIA WA CHUO KIKUU CHA MT. YOHANA KUSHIRIKI IBADA YA KUOMBOLEZA KIFO CHA MAKAMU MKUU WA CHUO HIKO PROF. GABRIEL MWALUKO


Mkuu wa mkoa wa Dodoma Dr. Rehema Nchimbi leo amewaongoza mamia ya wanajumuiya wa chuo kikuu cha Mt. Yohana Tanzania chenye makao yake makuu mjini Dodoma kushiriki ibada takatifu ya kuomboleza kifo cha makamu mkuuwa chuo hiko marehemu Prof. Gabriel Mwaluko.

Ibada hiyo takatifu ya maombolezo ilifanyika kwenye ukumbi wa chuo hiko mjini Dodoma ambapo ilihudhuriwa na uongozi na wanajumuiya wa chuo iko, ibada hiyo pia ilitumika kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa utumishi aliompa marehemu Prof. Mwaluko chuoni hapo, kwenye taasisi mbalimbali na kuitumikia jamii kwa ujumla enzi za uhai wake.

Akitoa taarifa kwenye ibada hiyo Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo cha Mt. Yohana Dr. Asad Kipanga alisema takribani miezi miwili marehemu Prof. Mwaluko alikuwa nchini India kwa matibabu na kwa kipindi chote hiko chuo kimekuwa na mawasiliano ya karibu na familia ya Prof. Mwaluko na walitarajia Prof. angerejea salama nchini siku za hivi karibuni lakini hali haikuwa hivyo.

Kwa upande wake mlezi wa kiroho chuoni hapo Askofu Francis Ntiruka akiongoza ibada hiyo amebainisha kua chuo na jumuiya yake  nzima imepata pigo kubwa na ameeleza watamkumbuka marehemu Prof. Mwaluko kama  mtu  wa imani kupitia maisha na matendo yake, pia atakumbukwa kujitolea kwake  katika kazi  na hamasa  yake. Askofu Ntiruka ametoa rai  kwa viongozi wa mataifa ya leo kuwa endapo watatumika kwa kujitoa  uongozi wao utadumu, utaheshimika na kukumbukwa daima ambapo alimtolea mfano baba wa taifa mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Nae Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr. Rehema Nchimbi aliyewaongoza wanajumuiya wa chuo kikuu cha Mt. Yohana  katika ibada hiyo amesema serikali imepokea msiba chuo wa prof. Mwaluko kwa majonzi na masikitiko kwa kutambua umuhimu aliokuanao Prof. Mwaluko kwenye hatua ya maendeleo iliyokuwa ikipitiwa na chuo hiko kwa sasa na kuongeza kuwa serikali inakitazama chuo hiko kwa upekee kwa mchango wake wa kuandaa wataalamu waliojifunza kuihudumia jamii kwa uadilifu.

No comments:

Post a Comment