Monday, November 25, 2013

AFNET WAZINDUA MAADHIMISHO YA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA KANDA YA KATI MKOANI DODOMA.

 
Polisi wa kike waliopo kwenye kitengo maarumu cha Dawati la ukatili wa
kijinsia wakiselebuka wimbo wa wanawake ulipigwa na kundi la FM
akademia la jijini Dar es laam wakati wa uzinduzi wa kupiga vita
vitendo vya ukatili.
Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserekali linalopiga vita vitendo vya
ukatili na unyanyasaji  wa kijinsia Sara Mwaga akifafanua jambo
alipokuwa akisoma risala wakati wa uzindizi wa wa maadhimisho ya
mpango huo, kulia ni Mgeni Rasmi Stephen Humbi na kushoto ni
Muwakilishi wa mkuu wa magereza [ASP] Shirima.
Baadhi ya wananchi waliohudhulia uzinduzi huo uliofanyika leo katika
viwanja vya nyerere Dodoma



Kikundi cha ngoma cha Hengo toka wilayani kongwa kikionyesha umahili
wa kuimba na kucheza wakati wa ufunguzi wa maadhimisho ya kupinga
vitendo vya ukatili wakijinsia yanayofanyika kuanzia Nov 25 mpaka Des
10 2013 mkoani Dodoma
 
Na John Banda, Dodoma
ASILIMIA %42 ya kesi zilizoripotiwa polisi kwa kipindi cha miaka minne ni za vipigo kwa wanawake hali inayodhoofisha afya jamii.
Takwimu hiyo iliyotolewa wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya kupinga ukatili wa kijinsia kanda ya kati ilitolewa na mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserekali linalopinga ukatili wa kijinsia na watoto [AFNET] Bi Sara Mwaga.
Mkurugenzi huyo alisema kesi zinazoongoza kupokelewa na jeshi la polisi mkoani hapa ni za vipigo hasa kwa wanawake vinavyofanywa na wenzi wao katika ndoa na walio katika mahusiano ya kimapenzi.
‘’Bi Sara alisema kuwa kesi za vipigo zinaongoza kwa asilimia 42, ikifuatiwa na Ubakaji 32.7%, Shamburio la mwili lenye 16.9%  wakati vitendo vya ulawiti ni 7.4.5. ambapo umepungua toka %15 ya mwaka 2012 hali hii inadhoofisha afya ya jamii’’, alisema
Aidha alisema pamoja na takwimu kuonyesha tatizo la ukatili wa kijinsia kuwa juu kitakwimu lakini hali halisi ni mbaya zaidi kuliko invyoonekana kutokana na kesi chache sana zinazoripotiwa kwenye vyombo vya dola hadi hivi sasa.
Alisema pamoja na hilo ni kesi chache kati hizo zinazoripotiwa zinazofikia mwisho na wahusika kuchukuliwa hatua zinazosihili, huku akibainisha kuwa tatizo ni watu kutoelewa haki zao na nini cha kufanya ili kuzidai.
Uzindizi wa Maadhimisho hayo yanayofanyika kwa siku 16 katika ukanda wa kati unashirikisha mikoa iliyoathirika kwa kiasi kikubwa na tatizo hilo la unyanyasaji na ukatili wa kijinsia ya Singida, Tabora na Dodoma  

No comments:

Post a Comment