Wednesday, February 6, 2013

RAIS KIKWETE AZINDUA UJENZI WA UWANJA WA NDEGE WA KIGOMA

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na viongozi wengine akikata utepe kuzindua  ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma leo Januari 4, 2013
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mkurugenzi mkazi wa Benki ya Dunia kwa nchi za Tanzania, Uganda na Burundi, Phillipe Dongier, wakifunua kitambaa kuashiria kuweka jiwe la msingi katika uzinduzi wa ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma leo .
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete, akiongozana na Mkurugenzi mkazi wa Benki ya Dunia kwa nchi za Tanzania, Uganda na Burundi, Phillipe Dongier, mkewe Mama Salma Kikwete, Waziri wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe pamoja na viongozi wengine baada ya uzinduzi wa ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma leo.
 Msanii Diamond na kundi lake wakishambulia jukwaa wakati wa sherehe za  uzinduzi wa ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma leo.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete, akisalimiana na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Muungano eneo la Kibaoni wilayani Uvinza, Kigoma, akiwa njiani kuelekea mjini Kigoma, akitokea kukagua ujenzi wa daraja la Mto Malagarasi leo.

No comments:

Post a Comment