Monday, September 30, 2013

WAZIRI WA INDIA ATUPWA JELA KWA TUHUMA ZA MATUMIZI MABAYA YA FEDHA ZA UMMA.


BIHAR, Jharkhand, India

Mahakama Kuu ya Ranchi nchini India imetoa hukumu 
kwa, Lalu Prasad (66), pamoja na washtakiwa wenzake 44 kwenda jela baada ya kupatikana na hatia ya rushwa wakati alipokuwa waziri mkuu wa Bihar. 

Kesi hiyo iliyovuta hisia za watu wengi Lalu alipatikana na hatia ya matumizi mabaya ya Rupia 37 crore alipokuwa waziri mkuu miaka 17 iliyopita. Hata hivyo hukumu hiyo itatangazwa siku ya Alhamisi kupitia video katika ukumbi wa mahakama hiyo.

Pia alipatikana na kashfa kubwa wakati akiwa kama mtumishi wa serikali kushindwa kuzuia matumizi mabaya ya fedha wakati akiwa waziri mkuu kiasi cha Rupia 950 crores zilizotumika kulipia bili za hewa katika matumizi ya madawa na chakula cha mifugo. Kufuatia hukumu hiyo Lalu amepoteza sifa ya kuwa mwanachama wa bunge, kwa mujibu wa hukumu ya Mahakama Kuu hivi karibuni.

Washtakiwa wengine ni pamoja na waziri wa zamani 
 Waziri Mkuu wa zamani Mishra Jagannath pia alipatikana na hatia katika mahakama hiyo ya Juu kabisa, pamoja na wanasiasa wengine sita, wawili ambao ni wa chama tawala cha Janata Dal-Muungano. 

Lalu alikuwepo katika mahakama na kuketi wakati hukumu dhidi yake ikisomwa mahakamani hapo, ambapo ametiwa hatia pamoja na watu wengine 44, ikiwa ni pamoja na wanasiasa saba zaidi na watendaji wa serikali wanne

No comments:

Post a Comment