Friday, May 31, 2013

WAZIRI MKUU AFUNGA SEMINA YA WAKUU WA MIKOA NA WILAYA KUHUSU UTARATIBU WA KUPATA MBOLEA YA RUZUKU KWA WAKULIMA.



Waziri Mkuu Mizengo Pinda akimfafanulia jambo  Mkuu wa Wilaya ya Bunda Angelina Mabula nje ya ukumbi wa Royal Village Dodoma walipoku wakitoka Kwenye Semina ya wakuu wa mikoa, Wilaya na Wabunge kuhusu Mfumo mpya wa utoaji wa Ruzuku ya Mbolea ya mazao kwa wakulima, iliyoandaliwa na Wizara ya kilimo na Chakula.




Waziri mkuu Mizengo Pinda akitoka kufunga Semina ya siku Mbili iliyofanyika Dodoma jana iliyowahusisha Wabunge, Wakuu wa Mkoa na Wilaya wa Nchi Nzima Kuhusu Utaratibu mpya wa Utoaji wa Ruzuku ya mbolea ya mazao kwa Wakulima katikati ni Waziri wa Kilimo na Chakula Christopher Chiza Naibu Waziri wa wizara hiyo Adamu Malima na Mkuu wa Wilaya ya Bunda Angelina Mabula




Washiriki wa Semina ya Utaratibu Mpya wa utoaji wa Ruzuku ya Mbolea Kwa wakulima iliyofanyika mjini Dodoma kwa siku mbili

                                         PICHA NA JOHN BANDA 
       

No comments:

Post a Comment