Sunday, May 25, 2014

HUU NDIO UKWELI WA BWANA HARUSI KUINGIA MITINI NA KUSABABISHA KUOTA MBAWA NDOA YA MH MBUNGE VICKY KAMATA

Mbunge wa Viti maalumu CCM, Vicky Kamata, akiwa amelazwa katika Hospitali ya Tabata General, jijini Dar es Salaam baada ya juzi kupatwa na ugonjwa ghafla wakati akijiandaa kuelekea Kanisani kwa ajili ya kufunga ndoa. Picha na Florence Majani 
HABARI zilizizoufikia mtandao huu zinasema kuwa Kilichotokea na kusababisha Bibi Harusi mtarajiwa Vick Kamata, kuanguka  na kuugua ghafla ni mshituko baada ya Bwana harusi kughaili ghafla kuendelea na wazo lake la kufunga ndoa.
Mtonyaji wa habari hizi ametonya kuwa ikiwa imebaki siku moja tu kufungwa ndoa hiyo, wapambe waliibuka na kumtafuta Bwana harusi na 'kumuuma sikio' yaani kumpa umbea ambao haukuweza kufahamika mapema kuwa ulikuwa ni wa aina gani huku ikidaiwa kuwa Bwana harusi alibadilika ghafla baada ya kukutana na watu hao na kuanza kuonyesha msimamo wake.
Wakati akiendelea na msimamo wake huo, ndipo ikamfikia Bi harusi na kushindwa kufikia muafaka huku Bwana harusi akiombwa kutoendelea na msimamo wake lakini hakuweza kubadili maamuzi, na ndiyo sababo hasa ya Bi harusi huyo kupatwa na mshituko.
Harusi hiyo iliyokuwa ifungwe jana Jumamosi, ilikuwa ni moja kati ya harusi zilizokuwa gumzo kubwa na ikitumia gharama kubwa zaidi jijini dar na hata nchini kote kuwahi kufungwa.
Cha kujiuliza ni kwamba hao wapambe hawakuweza kufanya umbea wao hadi ikiwa zimebaki dakika za majeruhi, na hata kama ni kweli hayo waliyomueleza Bwana harusi kama yalitokea huoni kama yalikuwa ni mchongo laamumu ulioandaliwa maalum???
Pamoja na haya yote lakini bado ukweli atabaki kuwa nao Bibi harusi na Bwana harusi kwa kile alichoelezwa na wapambe hao.

No comments:

Post a Comment