Sunday, May 4, 2014

AL-SHABAB WALIPUA TENA KENYA KATIKA MIJI YA NAIROBI NA MOMBASA NA KUUA WATU WA TATU HUKU 60 WAKIJERUIWA


 Mlipuko kadhaa imetokea mjini Mombasa nchini Kenya, ambapo imedaiwa walipuaji wamelipua sehemu tatu tofauti.
Akizungumza kutoa taarifa za tukio hilo Kamishna wa kaunti ya mombasa Nelson Marwa, amesema kuwa waliotekeleza shambulizi hilo huenda wametoroka wakitumia piki piki.

Aidha amesema kuwa watu 3 wamefariki kutokana shambulizi hilo la guruneti, huku mlipuko mwingine ukishuhudiwa katika eneo la Nyali Reef, lakini hakuna majeruhi.

Ikumbukwe kuwa shambulizi hili linajiri siku chache tu baada ya mlipuko mwingine kushuhudiwa jijini Nairobi katika kituo cha polisi cha Pangani ambapo watu 4 wakiwemo maafisa 2 wa polisi walifariki.

Msemaji huyo amesema kuwa maafisa wa polisi  tayari wameanza kuwasaka washukiwa wa matukio hayo.
Repoti kutoka Shirika la Msalaba mwekundu, inasema kuwa waliofariki ni watu watstu akiwamo mwanamke mmoja na wanaume wawili.

Wwalijeruhiwa 25,kwa sasa waliojeruhiwa wanaendelea na matibabu ikiwa ni pamoja na xray na ukaguzi mwengne.vioñgozi wa kaunti wa msa wamefika.
Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo wakiwa eneo la tukio.
Mmoja kati ya watu waliopoteza maisha katika tukio hilo.

No comments:

Post a Comment