Tuesday, January 7, 2014

ZITTO KABWE ASHINDA KESI YAKE ... AIBWAGA CHADEMA LIVE!!


Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Zitto Z. Kabwe pamoja na Mwanasheria wake,Albert Msando (kulia) wakiwasili katika Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam leo huku wakiongozana na wafuasi wanaopinga kuvuliwa uongozi wake,tayari kwa kwenda kusikiliza kesi yake aliyoifungua dhidi ya Chama Chake cha CHADEMA inayosikilizwa leo Mahakama Kuu.
**********
 
Mahakama kuu ya Tanzania imetengua maamuzi ya Chadema ya kumvua madaraka Zitto Kabwe.
Judge amesisitiza sana umuhimu wa demokrasia na kuvumiliana inapotokea tofauti ya mawazo. Amesema, kila mtanzania anastahili kusikilizwa na kupewa nafasi ya kuamua atakalo bila kuvunja katiba ya nchi. Kwa hiyo haoni iweje hawa Chadema, tena watatu watatu tu, mwenyekiti, katibu na mnadhimu mkuu wa chama ndiyo wawe miungu watu kwa kunyanyasa watao maoni chanya kuhusu mustakabari wa nchi kidemokrasia.

Judge kaamua kuwa kamati haitakuwa na mamlaka ya kujadili uanachama wake mpaka atakaposikilizwa na pingamizi lake na baraza ndio litakalo amua uanachama wake.

U]Kamati kuu ya chadema haitajadili uanachama wake au chombo chochote hadi kesi ya msingi isikilizwe

No comments:

Post a Comment