Monday, September 8, 2014

NEWS ALERT..: Ajali nyingine mbaya yatokea Gairo mchana huu,zaidi ya watu wanne wanasadikiwa kupoteza maisha

Ajali nyingine mbaya:Basi la Abiria linalofanya safari zake kati ya Dar es Salaam - Tabora limepata ajali mbaya sana mchana huu katika eneo la  Kiegeya,Gairo na kupelekea zaidi ya watu wanne kupoteza maisha huku wengine wakiwa wamejeruhiwa vibaya sana.Ni majonzi makubwa yametawala katika eneo hilo hivi sasa,huku juhudi za kuokoa miili na majeruhi zikiendelea kama inavyoonekana pichani.ni siku tatu tu zimepita toka ajali nyingine mbaya itokee huko Musoma na kupoteza maisha ya zaidi ya Watanzania 35.Ripota wa Globu ya jamii yupo eneo la tukio hivi sasa na taarifa kamili itawajia baadae kidogo.

No comments:

Post a Comment