Wednesday, January 28, 2015

MWENYEKITI WA CHAMA CHA WAFANYABIASHARA JONSON MINJA KIZIMBANI.

  
NA John Banda,Dodoma
MWENYEKITI wa Shirikisho la vyama vya Wafanyabiashara Nchini Jonson
Minja  amefikishwa Mahakama ya Mkoa wa Dodoma kwa Mashitaka mawili
ikiwemo la kuchochea Wafanyabiashara  wasilipe kodi ya Serikali.
Akisoma Mashitaka hayo Wakili wa Serikali Gogfrey Wambari mbele ya
Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Rebbeka Mbiru alisema mtuhumiwa alitenda
makosa hayo tarehe 6 Septemba 2014 alipokuwa katika mkutano na
Wafanyabiashara katika ukumbi wa Chuo cha Mipango Dodoma.
Wambari alisema Mtuhumiwa alitenda makosa mawili ya Kushawishi
Wafanyabiasha kutenda kosa la jinai na kosa la pili kuzuia ukusanyaji
wa Kodi kwa kutumia Mashine za Kielotroniki EFD.
‘’Kifungu cha 390 kinasomeka pamoja na kifungu cha 35 cha Sheria ya
adhabu sura ya 16 ni  kosa kushawishi vitendo vyovyote vya jinai’’
‘’Kifungu cha 107 kifungu kidogo C cha Sheria ya kodi sura ya 332 ya
mwaka 2004 ni kosa kuzuia ulipaji wa Kodi ya Serikali ‘’alisema
Wambari.
Aidha Wambari alimtaka Hakimu kuzingatia umbali wa anakoishi mtuhumiwa
wakati atakapokuwa akitoa masharti ya dhamana.
Kwa upande wake Mtuhumiwa wa Kesi hiyo Jonson Minja 34 alipoulizwa
makosa hayo na Hakimu alikana mashitaka yote.
Hata hivyo hakimu wa Mahakama hiyo Rebbeca Mbiru alitoa masharti ya
dhamana ya Mtuhumiwa kwa kusema kuwa anatakiwa awe na Wadhamini wawili
mmoja wapo akiwa mtumishi wa Serikali na wote wawili wawe na vitu

Mwenyekiti wa Shirikisho la wafanyabiashara Jonson Minja mwenye koti
akisindikizwa katika mahakama ya mkoa wa Dodoma Chini ya ulinzi wa
askari polisi.

No comments:

Post a Comment