Tuesday, April 22, 2014

MBUNGE SOMALIA AUWAWA KWA BOMU.

Polisi wa Somalia akiangalia mabaki ya mlipuko wa gari lililopigwa bomu huko Mogadishu, Somalia, Jumatatu, April, 21, 2014.
Walinda amani wa Umoja wa Afrika Somalia.
Walinda amani wa Umoja wa Afrika Somalia.
Mbunge mmoja wa Somalia ameuwawa kwa bomu lililokuwa limetegwa kwenye gari huko Mogadishu.
Isak Mohamed Ibrahim aliuwawa wakati bomu lililokuwa limefichwa kwenye gari yake lililpolika kwenye makao makuu ya wilaya ya Hamar Weyne.
Mbunge mwingine Mohamed Abdi alijeruhiwa katika shambulizi hilo. Shambulizi hilo na majeruhi vilithibitishwa na ofisi ya waziri mkuu wa Somalia .
Kundi la wanamgambo la Alshabab la Somalia limedai kuhusika na shambulizi hilo.
Kundi hilo limepoteza maeneo yake mengi iliyokuwa ikidhibiti katika miaka ya karibuni kwa majeshi ya Umoja wa Afrika na serikali ya Somalia. Lakini wanajeshi hao waliendelea kufanya mashambulizi ya kila mara .
Mwezi Februari watu 17 waliuwawa wakati wapiganaji wa Alshabab walipovamia ikulu ya rais. Rais Hassan Sheikh Mohamud hakujeruhiwa katika shambulizi hilo

No comments:

Post a Comment