Tuesday, February 17, 2015

MHE. CHIKU GALLAWA AKAGUA UJENZI WA MAABARA MANISPAA YA DODOMA, AMUAGIZA MKURUGENZI KUWACHUKULIA HATUA WATENDAJI WANAOSHINDWA KUSIMAMIA UTEKELEZAJI WA UJENZI WA MAABARA

 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Chiku Gallawa (mwenye kilemba kichwani) akimsikiliza Afisa Mtendaji wa Kata ya Msalato Dodoma  Ndg. Herman Malindira (kulia) akiwasilisha taarifa ya mradi wa ujenzi maabara kwenye sekondari ya Chikole Feb. 16, 2015.
 Mhe. Chiku Gallawa (kushoto) akitoa maagizo kwa viongozi wa Manispaa ya Dodoma na kata ya Msalato baada ya kutoridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa maabara wakati alipofanya ziara ya ukaguzi wa Maabara Mjini Dodoma Feb. 16, 2015.
 Mhe. Chiku Gallawa (katikati) akionesha kutokuridhishwa na hatua ya ujezi wa maabara kwenye sekondari ya Miyuji inayojengwa na Kata za Miyuji na Mnadani ikiwa hatua ya msingi wakati alipofanya ziara ya ukaguzi wa Maabara Mjini Dodoma Feb. 16, 2015, Amemuagiza Mkurugenzi Manispaa ya Dodoma kuwachukulia hatua watendaji wote walioshindwa kusimamia ujenzi wa maabara.
 Mhe. Chiku Gallawa (katikati) akiwaagiza viongozi wa Manispaa ya Dodoma na kata ya Chamwino kufanya kazi kwa kushirikiana na wananchi na wadau mbalimbali kuhakikisha wanakamilisha ujenzi wa maabara sekondari ya Chinangali ifikapo mwishoni mwa mwezi Aprili, Mhe. Gallawa ameonesha kutokuridhika na ujenzi wakati alipofanya ziara ya ukaguzi wa Maabara Mjini Dodoma Feb. 16, 2015 na kukuta maabara ik kwenye hatua ya ujenzi wa msingi.
Mhe. Chiku Gallawa (kushoto) akiwaagiza viongozi wa Manispaa ya Dodoma na kata ya Chang’ombe kuhakikisha wanakamilisha ujenzi wa maabara sekondari ya Lukundo ifikapo mwishoni mwa mwezi Aprili, Mhe. Gallawa ameonesha kutokuridhika na ujenzi wa Maabara Manispaa ya Dodoma wakati alipofanya ziara ya ukaguzi wa Maabara Feb. 16, 2015.

No comments:

Post a Comment