Tuesday, March 10, 2015

CHADEMA WAMFUKUZA RASMI UANACHAMA ZITO KABWE HIVYO SI MBUNGE TENA NA JIMBO LIKO WAZI.



Hatimaye Chama Cha Demokrasia na Maendeleo ( CHADEMA) kimeshinda kesi dhidi ya aliyekuwa mwanachama wake Zitto Kabwe.


Mahakama imeamua katika hukumu yake leo kuwa Chama kinaweza kuendelea na taratibu zake.


Aidha, Mahakama imeamuru Zitto alipe gharama zote za kesi.
Mwaka jana Zitto Kabwe aliweka pingamizi mahakamni kuzuia kikao cha Kamati Kuu kumjadili.

Hoja yake ni kupinga kuitisha kamati kuu kabla shauri lake kusikilizwa na Baraza Kuu.

Alidai anataka mahakama iagize kamati kuu ya CHADEMA kutojadili suala lake mpaka baraza kuu likae kuamua rufaa yake.

Jopo la wanasheria wa Chadema likiongozwa na Mhe.Peter Kibatala na John Mallya litaongea na wanahabari muda mfupi ujao.

Nimepita katika mitandao ya jamii hiki ndicho kimeandikwa na Wanachadema

Quote By Tumaini Makene View Post
Chama kimeshinda hila nyingine. Wanachadema wameshinda kesi mahakamani.

Kesi aliyofungua Zitto imefutwa mahakamani leo.

So Chama kinaweza kuchukua uamuzi wowote wa kinidhamu kwa kuwa hakuna zuio tena. Hakuna case.


Quote By Peter Kibatala View Post

Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Dar es Salaam leo hii tarehe 10 March 2015 imetupilia mbali case ya msingi iliyofunguliwa na Zitto Zubeir Kabwe dhidi ya CHADEMA. 
Mahakama Kuu (Mziray,Judge) amekubaliana na hoja zetu za pingamizi dhidi ya case hiyo kwamba ilifunguliwa bila kufuata utaratibu wa kisheria. Mahakama Kuu imeipa CHADEMA gharama zote za kuendesha case hiyo. Kwa maana hiyo hakuna shauri lolote Mahakamani kwa sasa kuhusu suala hilo.
 
The CHADEMA legal Crown is back where it belongs; Peter Kibatala, Tundu Lissu, John Mallya.
 
Tuliahidi ku-post habari hizi siku moja hata kama ingechukua muda gani, na tumetimiza ahadi yetu

No comments:

Post a Comment