Friday, April 14, 2017

RAIS MAGUFULI ASIKITISHWA NA MAUAJI YA ASKARI ,ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA IGP.

MAUAJI YA KUTISHA MKOANI PWANI ,MAJAMBAZI YAUA POLISI 7.OPARATION YA KUWASAKA WAUAJI YAANZA.


picha za baadhi ya askari waliouwawa


Na Mathias Canal, Dar es salaam

Askari wa jeshi la Polisi Mkoani Pwani Jana waliwaua watu wanne watuhumiwa  katika majibizano ya risasi Mara baada ya kutokea Mauaji ya Askari nane waliokuwa wanatoka kubadilishana Rindo katika Barabara ya Dar es salaam- Lindi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamishna wa Operesheni na Mafunzo (CP) Nsato Marijani Mssanzya wakati wa mkutano wake na waandishi wa Habari alisema kuwa 
Jana tarehe 13/04/2017 majira ya saa kumi na mbili na robo jioni maeneo ya Mkengeni, Kata ya Mjawa, Wilaya ya Kibiti, Mkoani Pwani, Majambazi ambao idadi yao haijafahamika wakiwa na silaha za Moto walishambulia kwa risasi gari la Polisi lenye namba PT 3713 Toyota Land Cruiser na kuwaua askari hao nane.

Kamishna Mssanzya amewataja askari waliouwawa katika tukio hilo kuwa ni A/INSP Peter Kigugu, F.3451CPL Fransis, F.6990PC Haruna, G.3247 PC Jackson, H.1872 PC Zacharia, H.5503 PC Siwale, H.7629 PC Maswi na H.7680 PC Ayoub.

Kamishna Mssanzya alisema kuwa katika tukio hilo majambazi hayo yalipora silaha saba zikiwemo SMG Nne na Long Range Tatu.

Ameeleza kuwa Mara baada ya tukio hilo hatua za Kiintelijensia na kiupelelezi zilichukuliwa na zilipelekea askari kufuatilia na kubaini maficho ya muda ya majambazi hao na katika majibizano ya risasi majambazi wanne waliuawa na bunduki nne kupatikana, Mbili zikiwa ni zile zilizoibiwa katika tukio la Mkengeni na bunduki mbili zikiwa Mali ya majambazi hayo.

Kamishina Mssanzya amewasihi wananchi wakati Jeshi la Polisi likiendelea kuwatafuta majambazi hao wao kuendelea kuwa watulivu na kuendelee kutoa taarifa kwa jeshi la Polisi zitakazosaidia ukamataji wa wahalifu hao

Tuesday, April 11, 2017

KIKAO CHA MAJADILIANO BAINA YA SERIKALI NA SEKTA BINAFSI MJINI DODOMA.

A
Waziri wa fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa TPSF Dkt. Reginald Mengi pamoja na makamu mwenyekiti TPSF Mr. Salum Shamte.
A 2
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage, (mwenye suti nyeusi), kushoto ni Mhe. Dkt), Philip Mpango Waziri wa fedha na Mipango, Dkt. Reginald Mengi Mwenyekiti TPSF, pamoja na Ndugu Salum Shamte Makamu mwenyekiti TPSF
A 1
Baadhi ya washiriki wa Kikao cha majadiliano baina ya serikali na sekta binafsi.

RAIS DKT.MAGUFULI AMEWAAPISHA WAJUMBE WA KAMATI MAALUM YA PILI YA WACHUMI NA WANASHERIA ITAKAYOCHUNGUZA MCHANGA WENYE MADINI

 VVV
VVV 1

Friday, March 31, 2017

WAZIRI MKUU WA ETHIOPIA AWASILI NCHINI NA KUPOKELEWA NA RAIS MHE.DKT. MAGUFULI



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na kumpokea mgeni wake Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Terminal One jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na mgeni wake Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Terminal One jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn akipiga ngoma mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam, Pembeni yake ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpigia makofi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn wakati nyimbo za mataifa mawili (Tanzania na Ethiopia) zikipigwa mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Terminal One jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn akishuka kwenye jukwaa kwenda kukagua gwaride la Heshma lililoandaliwa kwa ajili yake.
Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn akikagua Gwaride la heshma lililoandaliwa kwa ajili yake.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na mgeni wake Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wanahabari mara baada ya kumaliza mkutano wa pamoja na Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn aliyeambatana na ujumbe wake Ikulu jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn akifurahia jambo wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akizungumza na Wanahabari Ikulu jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn akizungumza na Wanahabari Ikulu jijini Dar es Salaam mara baada ya mkutano wake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimtambulisha Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Eng. John Kijazi kwa mgeni wake Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn Ikulu jijini Dar es Salaam.
Shamra shamra zikiendelea wakati wa kuwasili Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Terminal 2 jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn akikaribishwa kwa kupewa ua na mtoto Xyleen Mapunda mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Terminal One jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU.

RAIS MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA SPIKA JOB NDUGAI KUFUATIA KIFO CHA MBUNGE ELLY MACHA

Wednesday, March 29, 2017

RC MAKONDA AWEKWA KITI MOTO BUNGENI DODOMA.


 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akihojiwa Leo mbele ya kamati ya bunge
Na Ofisi ya bunge, Dodoma

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda leo amehojiwa na Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusiana na tuhuma za kuingilia haki, uhuru na madaraka ya Bunge.

Mhe. Makonda aliwasili Bungeni  Dodoma majira ya saa nne asubuhi kuitikia wito wa Kamati hiyo uliotokana na Azimio la Bunge  lililotolewa na Bunge, Februari 8, 2017  katika Kikao cha Nane cha Mkutano wa Sita wa Bunge ambapo amehojiwa na kamati hiyo kwa muda wa masaa matatu kuhusu tuhuma zinazomkabili.

Katika kikao hicho, Bunge liliazimia kwamba Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Makonda na Mkuu wa Mkoa wa Arumeru, Mhe. Alexander Mnyeti kuitwa mbele ya Kamati ya Bunge ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge baada ya Bunge ili kujibu tuhuma hizo.

Akizungumza mara baada ya Kamati hiyo kumaliza kazi yake, Mwenyekiti wa Kamati ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, Mhe. George Mkuchika alisema Kamati hiyo imekutana leo baada ya kuagizwa na Mheshimiwa Spika wa Bunge kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge.

“Tumefanya kikao hiki cha Kamati baada ya kuagizwa na Mhe. Spika kwa kuwa kwa Mujibu wa Kanuni zetu, Kamati hii inakutana pale tu inapoagizwa na Spika wa Bunge,” alisema.

Alisema Mhe. Spika aliiagiza Kamati hiyo imuite Mhe. Makonda mbele ya Kamati  kufuatia azimio hilo la Bunge lililopitishwa  na Bunge Februari 8, ambapo pamoja na mambo mengine Mkuu huyo wa Mkoa alitakiwa kufika mbele ya Kamati kujibu tuhuma hizo zinazomkabili.

Alisema kwa mujibu wa Azimio hilo, Mhe. Makonda alidaiwa kutoa kauli kupitia Televisheni ya Clouds akidai kwamba wabunge wanasinzia Bungeni jambo lililoonekana kwamba ni kudharau Bunge.

“Napenda kutoa taarifa kwamba Mhe. Makonda leo amekuja mbele ya Kamati na ametupa ushirikiano mzuri, tumepokea maelezo yake na Kamati imemaliza kazi yake,” alisema.

Alisema kama ilivyo utaratibu, Kamati yake itakabidhi taarifa yake kwa Mhe. Spika kwa mujibu wa Kanuni ambapo Spika ndiye atakaeamua namna ya kutoa raarifa kuhusu kazi ya Kamati hiyo.
Mwisho.