
Thursday, January 24, 2013
USIKU WA TARANGIRE WAFANA VILIVYO
Wanamuziki wa Bendi ya FM Academia wakionesha vitu vyao wakati wa Hafla ya usiku wa Tarangire iliyofanyika kwenye hifadhi hiyo ya Taifa.
Mkuu wa Mkoa Dodoma Dr. Rehema Nchimbi (mwenye kilemba/miwani), Mkuu wa Mkoa Manyara Elaston Mbwilo (kulia kwa Dr. Nchimbi) Uongozi na wafanyakazi wa Hifadhi ya Taifa Tarangire wakiserebuka kwa muziki wa Bendi ya FM Academia wakati wa hafla ya Usiku wa Tarangire iliyofanyika hifadhini hapo
Monday, January 21, 2013
UKUTA WA KITUO CHA MABASI CHA UBUNGO WAANGUKA NA KUHARIBU MAGARI ZAIDI YA 20

Baadhi ya magari yaliyoangukiwa na ukuta.

Magari mbalimbali yakiwa chini ya kifusi.

Gari aina ya Noah likiwa limegandamizwa na zege.

Hii ndiyo hali halisi ya tukio lilivyokuwa.

Gari aina ya Toyota likiwa limebonyezwa na zege.

Watu wakiangalia magari yao.

Kenyela akiongea jambo juu ya ajali hiyo.

likuwa ni hasara tupu.

Mh. Lowassa ahudhuria msiba wa mume wa Mbunge wa zamani wa Temeke, Mama Khadija Kusaga
Waziri
Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akimpa
pole mfiwa,Mama Khadija Kusaga wakati alipofika nyumbani kwake Keko
Maghorofani jijini Dar es salaam jana.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh.
Edward Lowassa akiwa katika mazungumzo na Mbunge wa Jimbo la Temeke,
Mh. Abbas Mtemvu wakati walipokuwa kwenye msiba huo jana jioni.
YALIYOJIRI MKUTANO MKUU WA MWAKA WA YANGA JANA, SENDEU, MWESIGWA WAFUTIWA UANACHAMA
Mwenyekiti
Mpya wa Club ya Yanga Africans, Yusuf Manji akifafanua baadhi ya mambo
mbalimbali kwenye mkutano huo,uliochanganua mambo mbalimbali zikiwemo
changamoto za timu hiyo, maendeleo ya Klabu hiyo pamoja na ujenzi wa
kiwanja kikubwa cha mpira maeneo ya Jangwani,jijini dar, Sahihisho la
katiba yao, masuala mbalimbali yanayohusiana na wanachama wao, ustawi wa
wanachama wao, mikataba baina yao na wadhamini wao na mambo mengine
mengi yaliyoongelewa.
Sehemu ya meza kuu ya mkutano huo ilivyokuwa.
Makamu mwenyekiti wa timu ya Yanga,Clement Sanga akitolea ufafanuzi moja ya jambo lililoulizwa na wajumbe wa mkutano huo.
Beki
mahiri wa Yanga, Shadrack Nsajigwa (kulia) akipeana mkono wa shukrani
na Mwenyekiti wa Yanga,Yusuf Manji mara baada ya kutajwa kuwa ndiye
mchezaji aliyedumu Yanga kwa muda mrefu miongoni mwa wachezaji waliopo
hivi sasa, na kuwa mchezaji mwenye nidhamu zaidi, hivyo alizawadiwa
barua ya shukurani na kitita cha shilingi milioni moja.
Pichani
juu na chini ni baadhi ya Wajumbe wa timu ya Yanga waliopata nafasi ya
kuuliza maswali mbalimbali kwa Kamati ya Utendaji,mbele ya wageni
waalikwa mbalimbali waliohudhuria mkutano huo.
Mwenyekiti
wa Yanga,Yusuf Manji sambamba na Makamu mwenyekiti wa timu hiyo,Clement
Sanga wakifatilia jambo kwa makini ukumbini humo.
Baadhi ya wachezaji wa timu ya Yanga pia walihudhuria mkutano huo uliohusu mikakati mbalimbali ya kuimarisha timu hiyo.
Baadhi ya Wazee wa baraza wa timu ya Yanga wakifautilia kwa makini yaliyokuwa yakijili kwenye mkutano huo mkuu wa Kihistoria.
Kocha
mpya wa timu ya Yanga,kutoka nchini Uholanzi Ernest Brandts nae
aliruhusiwa kutoa yake machache kuhusina na timu yake ya Yanga.
Baadhi
ya Wanachama wa Yanga waliofurika kwa wingi ndani ya mkutano mkuu wa
timu hiyo uliofanyika ndani ya bwalo la Maofisa wa Polisi,Oysterbay
jijini Dar es salaam mapema leo asubuhi na kumalizika mapema jioni ya
leo.
Msanii mahiri wa kizazi kipya, Barnaba, pamoja na wasanii wenzake kutoka THT wakitumbuiza kwenye mkutano huo.
Mtangazaji
machachari wa kipindi cha michezo,Clouds FM/TV Mbwiga Mbwiguke,
akiwaweka sawa wanachama wa Yanga waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano
wao mkuu wa Mwaka.
RAIS KIKWETE AWASILI UFARANSA
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na mke wa Rais wa Mali MamaTouré
Lobbo Traoré waliyekutana naye uwanja wa ndege wa Kimataifa Charles de
Gaulle jijini Paris, Ufaransa, baada ya kuwasili tayari kuanza ziara ya
kiserikali ya siku tatu.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwa na mke wa Rais wa Mali Mama Touré
Lobbo Traoré waliyekutana naye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Charles
de Gaulle jijini Paris, Ufaransa, baad ya kuwasili tayari kuanza ziara
ya kiserikali ya siku tatu.
Subscribe to:
Posts (Atom)















